Jumanne, 12 Aprili 2016

MSHITUKOOO!!! MADIWANI WA MANISPAA YA SHINYANGA MJINI WABARIKI MRADI WA KUELIMISHA MASHOGA NA MAKAHABA.


Wakati serikali ikiendelea na zoezi la kamata kamata ya wanawake wanaojihusisha na biashara ya ngono /kuuza miili yao ,madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga wameriruhusu Shirika lisilo la kiserikali la Rafiki SDO kuendelea kutoa elimu ya UKIMWI kwa wanawake wanaojihusisha na biashara ya ngono “machangudoa” na wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao “Mashoga”,
Madiwani hao wamebariki mradi huo uendelee kwa masharti matatu ya shirika hilo kutumia wataalam wa afya kutoa elimu ya Ukimwi ,kutoruhusu ndoa ya jinsia moja na kutowapatia mafuta ya vilainishi vinavyosaidia kupunguza michubuko wakati wa tendo la kujamiiana ili kuhamasisha ngono kwao kama ilivyoripotiwa hapo awali. 
Madiwani waliazimia kuliruhusu shirika hilo jana kwenye kikao cha dharura cha baraza lao likiwa na ajenda moja ya kupata ufafanuzi juu ya shughuli za Mradi wa Shirika hilo la utoaji wa Elimu ya Ukimwi kwa watu hao, baada kutoa tamko la kusitisha shughuli zake kwenye kikao kilichopita, kwamba Shirika la Rafiki linatakiwa litoe ufafanuzi wa kina kuhusu elimu hiyo ili kuepuka kukiuka tamaduni za kiafrika. 
Shirika hilo hapo awali lilizuiwa kufanya kazi zake mwezi Machi mwaka huu na Madiwani hao baada ya kupata taarifa ya kufanya kazi zake kinyemelea kwenye kata zao”bila kushirikisha madiwani” huku kukiwa na madai kuwa wanakusanya Machangudoa na Mashoga na kisha kuwahamasisha kuendelea kuuza miili yao pamoja na kuwapatia mafuta ya vilainishi wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao. 
Akitoa ufafanuzi , mkurugenzi wa Shirika la Rafiki Gerald Ng’ong’a, alisema elimu wanayoitoa kwa machangudoa na mashoga ni kuwazuia kuendelea na biashara hiyo na kuwahamasisha kujiunga kwenye vikundi vya ujasiriamali ili wajikwamue kiuchumi. 
“Mimi ni mkristo kamwe siwezi kubadili mila na desturi za kiafrika kwa sababu ya mzungu…mradi huu unatekelezwa katika mikoa 11 Tanzania...ndugu zangu siku zote linapotokea jambo yanazungumzwa mengi,kuna wengine wanakuwa hawaelewi matokeo yake kupotosha jamii”,alisema Ng’ong’a. 
“Naomba radhi kwa taarifa zilizoenezwa hapo awali kuwa tunafanya shughuli ya kuchochea ngono,kutetea mashoga pamoja na makahaba... Nakiri kuwa tulifanya kosa kutotambulisha mradi wetu kwa madiwani na kutoipatia taarifa ofisi ya mkurugenzi ,ninakiri hapo tulikosea ndiyo maana zikaenea kwenu taarifa ambazo ni za upotoshaji”, alieleza Ng’ong’a. 
(Kwa hisani ya Malunde 1 blog.)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni